Aidha timu hizo zimekubaliana kuunda timu ya pamoja ya wanawake ya mchezo wa mpira wa magongo ya kuteleza kwenye barafu, na ili kuongeza hamasa Korea Kaskazini itatuma mashabiki 230 kwa ajili ya michuano hiyo itakayofanyika mjini PyeongChang nchini korea Kusini.
Hata hivyo hayo ni maamuzi ya mkutano wa majadiliano uliotoa mapendekezo hayo ambayo juma lijalo utayawasilisha kwenye kamati ya kimataifa ya Olimpiki ili kuomba ridhaa ya kufanya hivyo siku ya ufunguzi wa mashindano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |