Wawekezaji wa Uganda wametakiwa kujiandaa kujinufaisha na fursa kwenye sekta ya mafuta na gesi nchini humo.
Katibu wa kudumu kwenye wizara ya, kawi Robert Kasande, amesema sheria nchini humo imetenga maeneo Fulani maalum kwa wawekezaji wa Uganda pekee.
Baadi ya fursa hizo ni pamoja na kuuza chakula, vifaa vya ujenzi kama vile chuma na kutoa huduma za usalama.
Kasande amesema hayo wakati wa ufunguzi wa warsha ya wauzaji bidhaa za mafuta na gesi mjini Kampala ilioudhuriwa na zaidi ya watu 1,000.
Uganda inatarajiwa kuanza kuuza mafuta yake kuanzia mwaka 2020.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |