Wakuu wa nchi zaidi ya 40 za Afrika na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres watahudhuria mkutano wa 30 wa kilele wa Umoja wa Afrika utakaofanyika Addis Ababa, Ethiopia.
Hayo yamesemwa na waziri wa mambo ya nje wa Ethiopia Workneh Gebeyehu alipokuwa akiongea na waandishi wa habari. Amesema viongozi hao wanatarajiwa kujadili masuala ya kisiasa na usalama yanayoathiri nchi za Afrika, na mageuzi ya umoja huo.
Umoja wa Afrika umetangaza mwaka huu kuwa mwaka wa kupambana na ufisadi barani Afrika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |