• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yafafanua mpango wake wa jumla kuhusu sera za uchumi katika Mkutano wa Davos

    (GMT+08:00) 2018-01-25 10:38:13

    Ofisa mwandamizi wa China Bw. Liu He amefafanua mpango wa ngazi ya juu wa China kuhusu sera za uchumi kwa miaka kadhaa ijayo kwenye mkutano wa Baraza la Uchumi Duniani WEF unaoendelea huko Davos, nchini Uswisi.

    Katika hotuba yake Bw. Liu amesisitiza umuhimu kuhakikisha uchumi wa China unatimiza maendeleo yenye ubora wa kiwango cha juu, badala ya kupata ukuaji wa kasi tu.

    Amesema kufanikisha mabadiliko hayo ni msingi kwa China kutunga sera zake za kiuchumi, kijamii, kimuundo na za mageuzi kwa miaka kadhaa ijayo, na kwamba wakati China inaendelea kufungua mlango, mabadiliko hayo mapya kwenye maendeleo yake yatatoa fursa kubwa kwa sekta mbalimbali mpya, sio nchini China tu, na bali pia kwa dunia nzima kwa ujumla.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako