Waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Wang Yi amefafanua mpango wa diplomasia wa China kwa mwaka huu. Akiwahutubia wanadiplomasia wa nchi za nje nchini China kwenye tafrija ya mwaka mpya, Bw. Wang Yi amesema China itaendelea kuhimiza ujenzi wa "Ukanda mmoja, njia moja" katika mwaka mpya, na kutekeleza makubaliano yaliyofikiwa kwenye mkutano wa kwanza Baraza la Ukanda mmoja na njia moja kwa Ushirikiano wa kimataifa, uliofanyika mwezi Mei mwaka jana hapa Beijing. Bw. Wang Yi pia amesema katika mwaka mpya China itaimarisha mtandao wa wenzi wake wa ushirikiano duniani, na kuendelea na juhudi za kujenga mfumo wa nchi kubwa, unaolenga kuleta utulivu na maendeleo yenye uwiano duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |