Timu ya taifa ya Rwanda ya mchezo wa baiskeli imeanza kufanya maandalizi mjini Musanze kwa ajili ya mashindano ya Afrika ya Baiskeli yanayoanza Februari 13 mjini Kigali nchini Rwanda.
Kocha mkuu wa timu hiyo Sterling Magnell atatumia maandalizi hayo kuteua kikosi kamili kitakachoshiriki ambacho kitagawanyika katika makundi manne, timu za vijana (wanawake na wanaume), na timu za wakubwa (wanawake na wanaume).
Mwaka jana, Katika mashindano kama hayo yaliyofanyika nchini Misri, timu ya taifa ya Afrika Kusini ndiyo iliibuka mabingwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |