Msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric amesema Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu UAE wamekubaliana na Umoja wa Mataifa kuhusu kutoa dola za kimarekani bilioni 1 ili kuisaidia Yemen inayosumbuliwa na vita. Amesema dola milioni 930 za mfuko huo kwa Umoja wa Mataifa zitatumiwa kutoa msaada wa kibinadamu ili kuunga mkono Mpango wa Msaada wa Kibinadamu wa Yemen YHRP kwa mwaka 2018, na dola milioni 70 nyingine zitatolewa na nchi hizo mbili ili kuunga mkono ukarabati wa bandari na miundombinu nchini Yemen.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |