Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto ,nchini Tanzania,Ummy Mwalimu amesema sekta ya utalii ina mchango mkubwa wa kukuza pato la mtu mmoja mmoja na la taifa kwa ujumla.
Ummy alisema hayo katika hotuba yake iliyosomwa na mkurugenzi wa watoto wa wizara hiyo,Margaret Mussai ,katika kongamano la wanawake kuhusu utalii,na kusisitiza kuwa sekta ya utalii ni mkombozi mkubwa kwa maendeleo ya mwanamke kwani kinachohitajika zaidi ni kujiamini na kuwa wabunifu.
Mussai aliwahamasisha wanawake kutumia fursa zilizopo kwenye utalii kujiletea maendeleo ya uchumi ndani ya familia zao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |