Katika droo iliyofanyika jana katika makao makuu ya Shirikisho la vyama vya soka Afrika CAF mjini Cairo, mabingwa wa soka nchini Uganda, klabu ya KCCA ambayo ndiyo timu pekee kutoka Afrika Mashariki iliyofuzu mechi za hatua ya makundi ya klabu bingwa Afrika, imepangwa katika kundi A ikiwa pamoja na timu za Township Rollers (Botswana), Esperance (Tunisia), na Al Ahly (Misri).
KCCA itaanza kucheza mechi yake katika hatua hiyo dhidi ya Township Rollers Mei 4 mwaka huu mjini Gaborone nchini Botswana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |