Tovuti ya wizara ya ulinzi ya Russia imekumbwa na mashambulizi ya wadukuzi kutoka kwa Ulaya magharibi, Amerika kaskazini na Ukraine. Wizara hiyo imesema jana ilifanya upigaji kura wa kuchagua majina ya silaha tatu mpya za Russia kwenye tovuti ya wizara hiyo, na tovuti hiyo ilishambuliwa mara saba, saa moja kabla ya kumalizika kwa upigaji kura huo. Wizara hiyo pia imesema kitengo cha usalama wa mtandao kimefanikiwa kuzuia mashambulizi hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |