Wizara ya mambo ya nje ya Iraq imelaani shambulizi lililofanywa na jeshi la Uturuki na kusababisha vifo vya raia kadhaa kwenye eneo la Suran kaskazini mwa Iraq. Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo inasema wizara hiyo inalaani mwendelezo wa mashambulizi dhidi ya raia wa kawaida kwenye jimbo la Kurdistan, na kusisitiza msimamo wake wa kupinga uwepo wa nguvu yoyote ya nchi jirani nchini Iraq, na kuipinga nchi yoyote jirani kufanya operesheni za kijeshi kwenye ardhi ya Iraq.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |