Rais Vladimir Putin wa Russia amesaini amri ya kutangaza siku moja ya maombolezo ya kitaifa kwa wahanga wa ajali kubwa ya moto iliyotokea katika jumba moja la maduka mjini Kemerovo, na kusababisha vifo vya watu 64. Leo bendera ya taifa itapepea nusu mlingoti, na vipindi vyote vya burudani katika radio na televisheni vitasimamishwa kote nchini Russia. Rais Putin pia imeitaka serikali kutoa msaada kwa familia za wahanga, na kuahidi kuwafikisha wahusika mbele ya sheria baada ya uchunguzi kuwatambua.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |