Waziri mkuu wa Iraq Bw. Haider al-Abadi amesema Iraq haitaki kujiingiza kwenye mgogoro kati ya Marekani na Iran. Akihutubia mkutano wa Baraza la nishati la Iraq uliofanyika jana mjini Baghdad, Bw. Al-Abadi amesema Iraq inataka kudumisha uwiano wakati wa kushughulikia uhusiano kati yake na Iran na Marekani, na kwamba kutojiingiza kwenye mgogoro kati ya Iran na Marekani kunalingana na maslahi ya Iraq. Bw. Al-Abadi pia ametoa mwito kwa Marekani kutojitoa kwenye makubaliano ya nyuklia ya Iran yaliyofikiwa mwaka 2015.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |