Bunge la Ethiopia leo limemuidhinisha rasmi Bw. Abiy Ahmed kuwa waziri mkuu mpya wa nchi hiyo.
Tarehe 27 Machi, chama tawala cha Ethiopia EPRDF kilichagua Bw. Abiy Ahmed kuwa mwenyekiti mpya wa chama hicho, ambacho kina idadi kubwa ya wabunge katika bunge la Ethiopia, na alitakiwa kuidhinishwa na bunge kabla ya kuchukua nafasi hiyo.
Abiy Ahmed alizaliwa mwaka 1976, alikuwa waziri wa sayansi na teknolojia wa Ethiopia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |