• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Libya yaanza kuwasaka wapiganaji waliosalia wa kundi la IS

    (GMT+08:00) 2018-04-03 18:16:23

    Serikali ya Libya imetangaza kuanza operesheni ya kijeshi ya kuwaondoa wapiganaji waliosalia wa kundi la IS, mashariki mwa Tripoli.

    Msemaji wa serikali ya umoja wa makabila Mohamed Al-Sallak amesema, kwa mujibu wa amri ya waziri mkuu wa Libya Fayez Serraj, operesheni hiyo iliyopewa jina la Homeland Storm imeanza jana na inalenga kuwasaka magaidi nchini humo hasa wapiganaji wa kundi la IS.

    Habari zinasema, vikosi vyote vya serikali vimeshiriki kwenye operesheni hiyo inayofanyika katika miji ya Misurata, Sirte, Bani Walid na Tarhouna.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako