Wafanyabiashara katika kanda ya Afrika Mashariki wamewalaumu maafisa wa mipakani kwa kutokuwa na habari husika na oparesheni za kibiashara.
Wamelalamikia kudhulimiwa, kutozwa ushuru wa juu na ukaguzi wa bidhaa zao katika maeneo ya mipakani.
Wanasema bado maafisa kwenye mipaka hawajafahamu kuhusu itifaki ya soko la pamoja na mambo yanayohusu ushuru kwa bidhaa za soko la kikanda.
Mkurungezi wa kampuni ya Tandaza Tanzania Ltd bibi Githinji amesema kuna bidhaa na huduma nyingi ambazo tayari zimeondolewa ushuru lakini mamlaka wa mipakani wameendelea kudai kodi .
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |