Raia wapatao elfu 40 wamerejea makwao kwenye eneo la Ghouta Mashariki, baada ya jeshi la Syria kutwaa karibu wilaya zote za eneo hilo. Kwa mujibu wa Shirika la habari la Syria SANA, katika siku za karibuni jeshi la Syria limeendelea na operesheni za kutegua mabomu yaliyotegwa na waasi kwenye eneo hilo, na kazi za kuondoa vifusi, kukarabati miundombinu kama vile barabara, hospitali na shule pia zinaendelea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |