• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Afrika Kusini yawa mwenyeji wa mkutano wa kupambana na ujangili

    (GMT+08:00) 2018-04-05 08:48:14

    Mkutano wa nne wa maofisa waandamizi wa ulinzi na usalama unaohusu kupambana na ujangili, umefanyika katika mbuga ya wanyama ya Kruger nchini Afrika Kusini.

    Mkutano huo wa siku mbili ulihusu maswala ya kisheria na kutafuta njia zinazofanana za kuwaadhibu wale wanaokutwa na hatia za ujangili. Katika mkutano uliopita wa maofisa hao, ilifahamika kuwa nchi mbalimbali za SADC zina adhabu tofauti kwa makosa ya ujangili.

    Baada ya majadiliano ya muda mrefu, nchi za SADC zimepitisha mkakati wa pamoja utakaohimiza juhudi za kupambana na ujangili na usafirishaji haramu wa wanyamapori.

    Katika miaka ya hivi karibuni eneo la SADC limeshuhudia ongezeko la biashara haramu ya wanyama na ujangili, hasa wa pembe za ndovu na faru.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako