Rais Donald Trump wa Marekani na waziri mkuu wa Iraq Bw. Haider al-Abadi wamefanya mazungumzo kwa njia ya simu na kusisitiza umuhimu wa kufanyika kwa mafanikio ya uchaguzi mkuu ujao wa Iraq,. Mazungumzo hayo yamekuja baada ya Iraq kupanga kufanya uchaguzi wa bunge Mei 12, ambao utakuwa ni uchaguzi wa kwanza baada ya kundi la Islamic State kutokomezwa nchini humo. Imefahamika kuwa wagombea wapatao elfu saba wakiwemo wanawake zaidi ya elfu mbili, watagombea viti 329 vya bunge kwenye uchaguzi huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |