Mamlaka ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Benina mjini Benghazi, mashariki mwa Libya imesitisha safari zote za ndege kutokana na masuala ya kiusalama. Ofisa habari wa uwanja huo amesema kupitia taarifa kuwa uamuzi huo umetolewa kutokana na mgogoro wa kugombea udhibiti wa uwanja huo na masuala yaliyopo ya kiusalama na ya kijeshi. Taarifa inasema uwanja huo utaendelea kufungwa hadi ufumbuzi wa masuala hayo utakapopatikana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |