• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais Xi Jinping asema China itaongeza uingizaji wa bidhaa ili kukidhi mahitaji ya wananchi kwa maisha bora

    (GMT+08:00) 2018-04-10 11:49:43

    Akihutubia Mkutano wa mwaka wa Baraza la Asia la Boao, rais Xi Jinping wa China amesema China haitafuti urali mzuri kwenye biashara ya kimataifa, na kutarajia kwa dhati kupanua uagizaji wa bidhaa kutoka nje.

    Rais Xi amedokeza kuwa mwaka huu China itapunguza kwa kiasi kikubwa kiwango cha ushuru wa forodha kwa magari na bidhaa nyingine zinazoagizwa kutoka nje, ili kukidhi mahitaji ya wanachi na kuharakisha mchakato wa kujiunga na Shirika la biashara duniani WTO.

    Rais Xi pia amezitaka nchi zilizoendelea kuacha hatua za kuweka vizuizi na kulegeza udhibiti wa uuzaji wa bidhaa za teknolojia ya juu kwa China.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako