• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Marekani yaanza kushambulia maeneo ya Syria, milipuko yasikika

    (GMT+08:00) 2018-04-14 11:20:01

    Marekani imeanza mashambulizi dhidi ya Syria katika mji mkuu wa Damascus kabla siku ya jumamosi ambapo milio mikali yenye miale miekundu ya mabomu ilionekana katika anga.

    Milio ya sauti za milipuko ilisikika katika mji mkuu huo katika maeneo yote, huku majeshi ya anga yaSyria nayo yakionekana kurusha makombora yake kutokea mlima Qasion, ambao unatazamamana na mji mkuu wa Damascus.

    Mwenyekiti wa umoja wa wanadhimu wakuu wa majeshi ya marekani Joseph Dunford jana ijuma alisema mashambulizi hayo yanalenga maeneo kadha ya nchini Syria ikiwemo kituo cha utafiti , ghala la silaha za kikemikali na vituo vingine vya kuhifadhia silaha.

    Katika hatua nyingine, kituo cha televisheni cha Syria kimetangaza kuwa majeshi ya anga ya Syria yanajibu mashambulizi ya majeshi ya pamoja ya Marekani, Ufarasna na Uingereza.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako