• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kiongozi wa NATO atafuta uungaji mkono wa Iran kwa mpango wa kutoa mafunzo kwa jeshi la Iraq

    (GMT+08:00) 2018-04-17 09:15:04

    Katibu mkuu wa Jumuiya ya kujihami ya nchi za magharibi NATO Bw. Jens Stoltenberg ametoa mwito kwa Uturuki kutoa mchango kwa ajili ya mpango wake wa kutoa mafunzo ya kupambana na ugaidi kwa vikosi vya Iraq. Bw. Stoltenberg amesema hayo alipokutana na viongozi wa Uturuki mjini Ankara mapema jana. Amesema NATO inategemea kuungwa mkono na Uturuki kuzindua mafunzo hayo kwa kuwa kati ya nchi zote wanachama wa NATO Uturuki imeshuhudia mashambulizi mengi zaidi ya kigaidi na kuwa na uzoefu mwingi zaidi wa kupambana na ugaidi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako