Serikali ya mkoa wa Jowzjan wa Afghanistan imethibitisha kuwa jeshi la nchi hiyo limewaua wapiganaji 31 wa kundi la Islamic State na kuwajeruhi wengine 16 kwenye operesheni ya msako iliyofanyika mkoani humo katika siku mbili zilizopita. Msemaji wa serikali ya mkoa huo amesema mpaka sasa jeshi la Afghanistan limetwaa vijiji vitano vilivyodhibitiwa na IS, na operesheni hiyo inayoshirikisha jeshi la anga na vikosi maalumu itaendelea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |