Serikali ya Sudan Kusini jana ilizindua kiwanda cha nguzo za saruji kilichojengwa na kampuni ya China, kitakachowezesha mradi mkubwa wa kampuni ya China wa kukarabati na kupanua Mfumo wa Usambazaji wa Umeme mjini Juba.
Waziri wa Mabwawa na Umeme wa Sudan Kusini Bw. Dhieu Mathok amesema kuwa, kiwanda hicho kilichokodiwa na Power China, kitatengeneza nguzo 13,350 kwa ajili ya mradi wa usambazaji wa umeme katika mji mkuu na majimbo mengine.
Bw. Mathok amesema, majukumu makuu ya mradi huo ni kuongeza uwezo wa usambazaji wa umeme huko Juba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |