• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Waziri mkuu mpya wa Guinea Bissau ateuliwa

    (GMT+08:00) 2018-04-17 10:09:31

    Rais wa Guinea Bissau amemteua rasmi Bw. Aristides Gomes kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo, na kazi muhimu ya Bw. Gomes itakuwa ni kuunda serikali na kujiandaa kwa uchaguzi wa bunge.

    Habari kutoka ikulu ya Guinea Bissau zinasema uteuzi huo umefanyika baada ya makubaliano kufikiwa kati ya vyama vikubwa nchini Guinea Bissau, hasa Chama cha Uhuru wa Waafrika wa Guinea na Cape Verde na Chama cha Mageuzi ya Jamii, wakati wa Mkutano wa Lome wa Jumuiya ya kiuchumi ya nchi za Afrika Magharibi ECOWAS.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako