Klabu ya Rayon Sports ya Rwanda imewasili nchini Tanzania kwa ajili ya kuwakabili wenyeji Young Africans kwenye mchezo wa pili wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika utakaopigwa Mei 16 mjini Dar es Salaam.
Katika mchezo wake wa kwanza Rayon ilipata sare ya goli 1-1 dhidi ya Gor Mahia FC ya Kenya, na wenzao Young Africans wakipoteza kwa magoli 4-0 dhidi ya USM Algiers ya Algeria.
Mechi nyingine ya kundi D itapigwa mjini Nairobi, ambapo USM Algiers ambao wanaongoza kundi D, na tayari wamewasili nchini Kenya, watacheza na wenyeji wao Gor Mahia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |