Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Mike Pompeo amesema Marekani haitavumilia jaribio lolote la Russia kuingilia kati chaguzi za kipindi cha kati za Marekani zitakazofanyika Novemba na itachukua hatua madhubuti kuizuia Russia kufanya hivyo. Rais Donald Trump wa Marekani amekanusha uwepo wa uingiliaji wa Russia kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2016, na Russia pia imekanusha mara nyingi shutuma hizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |