• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kaunti zatumia fedha nyingi kwa mishahara

    (GMT+08:00) 2018-05-24 19:43:32

    Kaunti zimeendelea kutumia pesa zaidi kulipa mishahara na marupurupu kulingana na ripoti mpya kutoka kwa Mdhibiti wa Bajeti.

    Data ya miezi sita kutoka Desemba inaonyesha kuwa kaunti zilitumia asilimia 70 ya bajeti zao kulipa mishahara.

    Mdhibiti wa bajeti Bi Agnes Odhiambo alisema kiwango cha matumizi hayo ni Sh66.4 bilioni kutoka Sh61.8 bilioni katika kipindi hicho mwaka jana,

    Hicho ni kiwango cha juu zaidi cha matumizi ya bajeti kulipa mishahara tangu ugatuzi kuanza kutekelezwa.

    Kiwango hicho kimezidishwa na ongezeko la marupurupu kwa wafanyikazi wa kaunti ambapo Kaunti ya Tharaka Nithi iliongoza kwa asilimia 94.4 ya matumizi ya pesa kwa marupurupu na kufuatwa na Meru kwa asilimia 92.5 na Embu kwa asilimia 86.5, alisema mdhibiti huyo.

    Lakini Nairobi ilitumia pesa nyingi zaidi(Sh6.63 bilioni) na kufuatwa na Kakamega(Sh2.69 bilioni na Kiambu(Sh2.46 bilioni).

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako