Wizara ya afya ya Uganda imekanusha habari kuhusu kuwepo kwa mlipuko wa homa ya Ebola nchini humo. Taarifa iliyotolewa na waziri wa afya wa Uganda Bibi Sarah Opendi, inasema mwanamume mmoja mwenye umri wa miaka 35 alifariki Mei 21 kwenye eneo la Kakumiro, kutokana na homa ya Crimea-Kongo CCHF, na sio homa ya Ebola. Taarifa inasema wizara ya afya ya Uganda ina wasiwasi na ripoti kuhusu mlipuko wa Ebola kwenye eneo la Mubende nchini humo, na inataka kuujulisha umma kuwa hakuna maambukizi yoyote ya Ebola nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |