Rais Xi Jinping wa China ataendesha mkutano wa kilele wa 18 wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai SCO.
Waziri wa mambo ya nje wa China Wang Yi amesema mkutano huo unatarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 9 hadi 10, Juni mjini Qingdao, mashariki mwa China.
Viongozi wa nchi wanachama na nchi waangalizi wa SCO pamoja na wakuu wa mashirika husika ya kimataifa watahudhuria mkutano huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |