Aliyekuwa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ameshindwa kujitokeza bungeni kwa mara nyingine, kutoa maelezo kuhusu taarifa aliyotoa mwaka 2016 inayodai kuwa Zimbabwe inaweza kula hasara ya dola bilioni 15 za kimarekani kutokana na uvujaji wa mapato ya biashara ya almasi. Msemaji wa kamati ya madini na nishati ya bunge Bw. Themba Mliswa amesema bunge litatoa barua ya tatu na ya mwisho kumwalika Bw. Mugabe, na kama akikataa tena, atakabiliwa na mashtaka ya kupuuza bunge.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |