Baada ya kuwashinda Uganda kwa alama 34-16 kwenye michuano ya kombe la Elgon mjini Kampala, timu ya taifa ya Kenya imepanda katika msimamo wa viwango vya ubora duniani.
Kenya sasa imepanda kutoka nafasi ya 30 hadi 28, katika msimamo wa ubora wa mchezo huo duniani.
Wakati Kenya ikipanda, Uganda wao wameporomoka kwa nafasi mbili kutoka nafasi ya 35 waliyoshikilia hapo awali hadi nafasi ya 37.
Kenya na Uganda zitashiriki kwenye michuano ya kombe la Afrika la Raga inayotarajiwa kuanza ramsi mwezi ujao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |