Balozi wa Marekani kwenye Umoja wa Mataifa Nikki Haley, amesema Marekani itapiga kura ya veto muswada wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ulioandaliwa na Kuwait kuhusu ulinzi wa raia wa Palestina.
Bi. Haley amesema muswada huo una mtazamo wa upande mmoja ambao utasaidia kupunguza juhudi zinazoendelea za kuleta amani kati ya Israel na Palestina.
Kuwait, ambayo sio mjumbe wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, imesambaza muswada huo kwa nchi wajumbe wiki mbili zilizopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |