• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Watu 10 wafariki katika ajali ya barabarani magharibi mwa Tanzania

    (GMT+08:00) 2018-06-06 19:29:17

    Watu 10 wamefariki papo hapo na wengine 23 kujeruhiwa leo baada ya basi kugonga treni ya mizigo katika mkoa wa Kigoma, magharibi mwa Tanzania.

    Kamanda wa polisi mkoani Kigoma Martin Otieno amesema, basi hilo lilitupwa mita 100 kutoka kwenye eneo la ajali. Amesema waokoaji wamewatoa watu walionaswa kwenye mabaki ya basi hilo, na kwamba huenda idadi ya watu waliofariki ikaongezeka.

    Kamanda Otieno amesema, basi hilo lilikuwa likitokea Kigoma mjini kuelekea mkoani Tabora, katikati ya Tanzania, huku treni hiyo ya mizigo ikitokea Dar es Salaam kuelekea Kigoma. Amesema uchunguzi unaendelea ili kujua chanzo cha ajali hiyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako