Shirika la uhamiaji la kimataifa IOM limesema jumla ya wahamiaji 46 wamekufa maji katika pwani ya Yemen, wakati wakijaribu kuvuka bahari kutoka Pembe ya Afrika kwenda Yemen na Eneo la Ghuba kutafuta ajira. Taarifa iliyotolewa jana na IOM inasema wafanyakazi wake wako kwenye eneo la tukio kutoa misaada kwa watu walionusurika, na wamethibitisha kuwa kati ya wahanga, kuna wanaume 37 na wanawake 9, na wengine 16 bado hawajulikani walipo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |