Taasisi ya sayansi za kutafuta ushahidi ya taifa ya Guatemala imesema idadi ya vifo kutokana na mlipuko wa volkano ya Fuego imeongezeka na kufikia 99 baada ya miili mitatu zaidi kupatikana jana. Mlipuko huo mkubwa ulitokea Jumapili, na hadi kufikia Jumanne watu karibu 200 walikuwa hawajulikani walipo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |