Mabaki ya ndege ndogo iliyopotea katika msitu wa Aberdares katikati ya Kenya jumanne wiki hii yamepatikana mapema leo.
Katibu wa Kudumu wa Wizara ya Uchukuzi nchini Kenya Paul Maringa amesema, ndege hiyo imegunduliwa na timu ya waokoaji kwa kutumia ndege.
Ndege hiyo, Fly-SAX, iliyokuwa na abiria 10, wakiwemo wahudumu wawili, ilikuwa ikitokea uwanja wa ndege wa Kitale magharibi mwa Kenya kuelekea mjini Nairobi ilipopoteza mawasiliano na chumba cha uongozaji wa ndege.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |