Hilo limebainishwa na meya Isaya Mwita alipozungumza na wanahabari kuhusu mikakati ya kuutumia ukuta huo wenye urefu wa mita 920 pembezoni mwa Barabara ya Barrack Obama.
Miongoni mwa mipango iliyopo, Mwita alisema ni kuifanya sehemu hiyo iwe forodha kama ile ya Zanzibar ambayo watu hupumzika huku wakipata huduma mbalimbali.
Naye katibu mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Joseph Malongo alisema ukuta kama huo umejengwa Zanzibar na Tanga kwa zaidi ya Dola 5 milioni za Marekani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |