Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Jerry Qi, aliyasema hayo jana wakati akielezea mikakati ya kiwanda hicho ambacho kilianza kufanya kazi nchini Tanzania mwaka 2013.
Alisema kuwa awali walisimamisha uzalishaji kwa sababu walipungukiwa na malighafi lakini sasa wana pamba na mbegu za alizeti za kutosha na wameanza kufanya kazi hivi karibuni.
Aliongeza kuwa tangu kuanza kwa uzalishaji wamekuwa wakisaidia jamii inayowazunguka kama vile kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa maabara kwa shule za sekondari na kutoa zana za kilimo kwa wakulima wa wilaya ya Kishapu.
Qi aliongeza kuwa mafuta yanayozalishwa katika kiwanda hicho yamekuwa yakiuzwa nchini, Kenya na China na kwamba wamejipanga kuzalisha kiwango kikubwa cha mafuta kwa kutosheleza mahitaji ya wananchi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |