Maofisa 8 wa usalama wa Kenya wameuawa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kukanyaga bomu la kutengenezwa kienyeji katika kaunti ya Wajir.
Mratibu wa eneo la kaskazini mashariki Bw. Muhammed Saleh amethibitisha kuwa tukio hilo limetokea Bojigaras na kulishutumu kundi la Al Shabaab kuwajibika na shambulizi hilo. Amesema waliofariki ni pamoja na polisi watano na wengine watatu wa akiba.
Tukio hilo limetokea wakati tarehe sita June polisi wa Kenya walitahadharisha kuwa wapiganaji wa kundi la Al Shabaab wanapanga kufanya mashambulizi dhidi ya miundombinu muhimu kwenye eneo la kaskazini mashariki mwa Kenya ikiwemo mikoa ya pwani wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |