• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • UNHCR yapongeza hatua za Hispania za kukamilisha msukosuko wa uokoaji baharini

    (GMT+08:00) 2018-06-18 09:35:21

    Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limepongeza hatua zilizochukuliwa na Hispania kutatua msukosuko wa uokoaji katika bahari ya Mediterranean baada ya meli ya "Aquarius" iliyokuwa na wahamiaji zaidi 600 waliookolewa, kutoruhusiwa kutia nanga na kushusha wahamiaji nchini Italia na Malta.

    Kamishna mkuu wa UNHCR Bw. Filippo Grandi amefurahi kuona msukosuko huo umetatuliwa, lakini amesema tukio hilo halikutakiwa kutokea.

    Wahamiaji zaidi 600 waliookolewa wamehamishwa kutoka kwenye meli ya "Aquarius" na kwenda kwenye meli nyingine mbili za Italia, na kuwasili jana katika bandari ya Valencia, mashariki mwa Hispania.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako