Wapiganaji wa kundi la Taliban wameanza tena mashambulizi dhidi ya jeshi la Afghanistan baada ya makubaliano ya kusimamisha vita kwa siku tatu kumalizika jana usiku.
Msemaji wa mkoa wa Faryab ulioko kaskazini mwa Afghanistan Abdul Karim Yurash amesema, wapiganaji wa kundi hilo walishambulia vituo kadhaa vya ukaguzi katika wilaya mkoani humo mapema leo, na mapambano bado yanaendelea.
Serikali ya Afghanistan ilitangaza kusimamisha mapigano kuanzia tarehe 12 hadi 19 ili kulishawishi kundi la Taliban kuunga mkono mchakato mwafaka wa kitaifa. Kwa kujibu wa hatua hiyo, kundi hilo lilitangaza kusimamisha vita kwa siku tatu kuanzia Ijumaa iliyopita, na kumalizika jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |