Wizara ya ulinzi ya Marekani imetangaza kusitisha mpango wa mazoezi ya pamoja ya kijeshi na Korea Kusini yaliyopangwa kufanyika mwezi Agosti. Msemaji wa wizara hiyo Bibi Dana White amesema uamuzi huo unalingana na ahadi ya rais Donald Trump, aliyotoa wakati alipokutana na kiongozi wa Korea Kaskazini Bw. Kim Jong Un wiki iliyopita nchini Singapore.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |