• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa China atoa maagizo muhimu baada ya ajali ya meli nchini Thailand

    (GMT+08:00) 2018-07-06 20:49:09

    Rais Xi Jinping wa China ametoa maagizo muhimu kwa Wizara ya mambo ya nje ya China na ubalozi wa China nchini Thailand kuitaka serikali na idara zinazohusika za Thailand kutafuta na kuokoa watu waliopotea, na kuwapatia matibabu majeruhi katika ajali ya meli iliyotokea jana huko Phuket, Thailand.

    Habari zinasema meli mbili za utalii zilizobeba watalii kutoka China zilikumbwa na mvua kubwa na kuzama kwenye eneo la bahari karibu na kisiwa cha Phuket, hapo jana.

    Hadi sasa kati ya watalii 127, 16 wamekufa, wengine 33 hawajulikani walipo, na 78 waliokolewa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako