Reli ya mjini ya mji mkuu wa Nigeria, Abuja iliyojengwa na kampuni ya China ya CCECC imeanza kazi rasmi jana.
Akihutubia uzinduzi wa reli hiyo, rais Muhammadu Buhari wa nchi hiyo amesema, usafiri ni msingi wa mji, na serikali yake itaendelea kuongeza ujenzi wa usafiri wa mji. Pia rais Buhari ameshukuru uwekezaji wa China nchini Nigeria katika maendeleo ya uchumi na kuisifu kampuni hiyo kwa kumaliza ujenzi wa reli hiyo kwa wakati na kwa kiwango cha juu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |