Katibu mkuu wa Chama cha Jubilee ambacho ni chama tawala cha Kenya Bw. Raphael Tuju amesema Kenya inatarajia kujifunza kutoka chama cha kikomunisti cha China CPC katika baraza lililofanyika jana mjini Nairobi.
Bw. Tuju amesema chama cha CPC kimeweza kuiunganisha nchi yenye watu bilioni 1.3 kuleta maendeleo ya kiuchumi na ya kijamii, hivyo chama chake kinataka kujifunza kutokana na uzoefu huo mzuri.
Naibu Mtendaji mkuu wa Kamati ya Mkoa wa Guangxi katika Shule ya chama cha CPC Bw. Huang Jian hua amesema, vyama vya kisiasa vinahitaji kuimarisha kanuni za CPC miongoni mwa maofisa wa chama hicho, ili wasisahau lengo la kuboresha maisha ya wananchi wa kawaida.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |