Mwanariadha Solomon Lekuta wa Kenya ameshinda medali ya dhahabu baada ya kushika nafasi ya kwanza kwenye mbio za mita 800 kwa upande wa wanaume kwenye mashindano ya dunia kwa vijana chini ya miaka 20 yanayoendelea mjini Tampere nchini Finland.
Kutokana na Lekuta aliyeshinda jana, pamoja na Edward Zakayo aliyeshinda dhahabu katika mbio za mita 5000, timu ya taifa ya Kenya sasa inajikusanyia medali sita dhahabu, ikiwa ni nyingi zaidi kuliko timu yoyote ile, na kuifanya iongoze kwenye msimamo wa mashindano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |