Nyota wa kimataifa wa Ureno, Cristiano Ronaldo jana amewasili mjini Turin nchini Italia kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kujiunga rasmi na timu ya Juventus ambayo ataitumika kwa mkataba wa miaka minne.
Baada kuwasili mjini Turin, Ronaldo alikwenda katika hospital maarufu iliyoko karibu na klabu hiyo ya J Medical Centre kwa ajili ya vipimo vya afya, na akitoka hospitalini hapo alilakiwa na maelfu ya mashabiki wa klabu hiyo waliokuwa nje ya hospitali kumsubiri.
Na baadaye alikutana na waandishi wa habari, kocha mkuu wa timu hiyo Massimiliano Allegri, pamoja na wachezaji wengine wapya wa klabu hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |