Maelfu ya wasyria wataondoka miji ya Kafraya na Foa inayozingirwa na waasi kaskazini magharibi mwa Syria, chini ya makubaliano mapya yaliyofikiwa kati ya serikali na waasi. Miji hiyo miwili ya washia ambayo imezingirwa kwa miaka mitatu, itashuhudia kuondoka kwa maelfu ya watu baada ya makubaliano mapya kufikiwa. Televisheni ya taifa imesema mji wa Ishtabrak ulioko kaskazini mwa mkoa wa Idlib pia unahusishwa kwenye makubaliano, ambako waasi wanatarajiwa kuachia huru watu waliotekwa kutoka miji hiyo. Imefahamika kuwa kazi ya kuwahamisha watu kutoka miji hiyo huenda itaanza leo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |